DC Manyoni aifuta amri yake mwenyewe ya kuwataka wananchi kuchangia shughuli za maendeleo.


Siku moja baada ya mkuu wa mkoa wa Singida kufuta amri halali ya mkuu wa wilaya ya Manyoni ya kuchangia shughuli za maendeleo na inayo wataka wakazi wote wenye umri wa miaka kumina nane kuchangia shililingi elfu kumina tano kwa mwaka,mkuu wa wilaya ya Manyoni naye amefuta rasmi amri yake aliyoitoa Septemba sita mwaka huu
.

Akiongea na waandishi wa habari mkuu wa wilaya ya Manyoni Bwana Geofrey Mwambe amesema amri hiyo ambayo ilitolewa mwaka 2013 na mkuu wa wilaya aliye kuwepo awali na yeye kuamua kuitekeleza,ameifuta rasmi baada ya agizo la mkuu wa mkoa wa Singida kufuta amri hiyo.

Katika hatua nyingi Bwana Mwambe amesema taarifa zilizotolewa katika mitandao ya kijamii ni uzushi na yeye na wakurugenzi wake hawajawahi kupokea malalamiko ya mtu kulazimishwa kuchangia shuguli za maendeleo au kupewa adhabu ya kufungwa.

Octoba 21 mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Methew Mtigumwe alitoa taarifa kwa vyombo vya habari ya kumwagiza mkuu wa wilaya ya Manyoni Bwana Geoffrey Mwambe kufuta amri inayo husu wakazi wa wilaya ya Manyoni kuchangia pesa kwa ajili ya shuguli za maendeleo. 

Chapisha Maoni

0 Maoni