Umoja wa Mataifa, al maarufu kama UN. Nini maoni ya Mugabe?

   Tofauti na rais Mugabe, viongozi wengine pia waliukosoa vikali sana umoja huu akiwemo dikteta  Adolph Hitler kipindi hicho ukiwa kama League of Nations ambao, pamoja na kuwa chini ya mwavuli wa kulinda amani,
Hitler alichukulia kama umoja kandamizi kwa Nchi adui wa Marekani, kama Ujerumani.


             Kwa kipindi kirefu pia, rais Mugabe amekuwa akiukosoa sana umoja huu hasa kushindwa kutatua migogoro mikubwa kama ule wa Palestine na Israel ambao umedumu kwa miaka kadhaa sasa toka 1948 baada ya Israel (kihistoria) kuzaliwa. Pamoja na mengine mengi, rais Mugabe amekuwa akionesha ari ya kuwataka waafrika hata kujitoa uanachama wa Umoja wa Mataifa kwa kile ambacho amekuwa akikiita kuwa waafrika tumefanywa kuwa wajumbe wa muda wa Umoja huo. Hali kadhalika, Mugabe pia amekuwa akiutaka uongozi wa Umoja huu wa kimataifa kulifanyia marejeleo shirika la ulinzi la Umoja wa mataifa ili kulifanya liwe na wajibu sawia katika kusimamia usalama bila kujali mipaka ama vigezo vingine vya nchi.

              Mugabe pia katika moja ya hotuba yake mjini Addis Ababa, alimtaka katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwatetea waafrika ili wapate haki sawa na mataifa mengine yanayojipa ukuu. Tujikumbushe hotuba hiyo ya rais Mugabe.

Chapisha Maoni

1 Maoni

  1. Acha maoni yako ya nini kifanyike ili blog iendelee

    JibuFuta

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA