Kikwete: Watu wananilisha maneno, mimi namuunga mkono rais Magufuli na Serikali yake

Aliyekuwa rais wa Tanzania Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, amesikitishwa na tabia ya watu kumlisha maneno ambayo hajasema hasa watu wa mtandaoni. Anaomba aachwe apumzike.



"Nasikitishwa na matumizi mabaya ya picha zangu mtandaoni hususani watu kunilisha maneno kutaka kutimiza malengo yao ya kisiasa.

Nimestaafu naomba niachwe nipumzike. Nisingependwa kuhusishwa na siasa za mtandaoni dhidi ya Serikali. Namuunga mkono Rais na Serikali yake"

Hivi karibuni Kikwete alinukuliwa akitoa kauli tata iliyizua gumzo mtaani hasa pale aliposema
"Ukiwa Kiongozi mpya ni lazima uonekane kweli mpya na mambo yako yawe mapya". 

Chapisha Maoni

0 Maoni