Prof Mbarawa aishukia Manajimenti ya Mamlaka Viwanja vya Ndege,waliojaliwa bila vigezo kutemwa.

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, ameitaka Bodi mpya ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kusimamia Menejimenti ya Mamlaka hiyo katika Idara ya Utawala na Rasilimali Watu kuhakikisha ajira zote zinazotolewa zinazingatia sifa na vigezo vya kuajiri.


Akizungumza katika uzinduzi wa Bodi hiyo mpya jijini Dar es Salaam jana pamoja na mambo mengine, Profesa Mbarawa aliisisitiza bodi hiyo kuifanyia kazi Ripoti ya Uchunguzi wa uendeshaji wa viwanja hivyo nchini na kufanya mabadiliko mara moja.

“Nataka muipitie ripoti niliyomkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mkuu na mfanyie maamuzi, suala la kuajiri watu kiholela, ninataka wote walioandikwa kwenye ripoti hiyo kuwa hawana sifa watolewe wapishe watu wenye sifa ili waweze kufanya kazi”, alisema.

Aidha, Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kusimamia kwa uadilifu miundombinu yote ya viwanja vya ndege nchini na kuhakikisha mashine za ukaguzi zinafanya kazi saa 24 ili kudhibiti mianya yote ya rushwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Ninatubu Lema alimhakikishia Waziri huyo kuwa ataongeza ushirikiano na wafanyakazi wote na kusimamia maagizo yote yaliyotolewa.

Chapisha Maoni

0 Maoni