Kituo cha Haki za sheria za binadamu LHRC kimelaani kitendo cha kukamatwa kwa mwanzilishi wa jamiiforums.


Kituo cha Sheria za Haki za Binadamu(LHRC) na Kituo cha Utetezi wa Haki za Binadamu(THRDC) kimelaani na kukemea kukamatwa na kuwekwa kizuizini Mkurugenzi wa JamiiForums, Maxence Melo.

Vituo hivyo vimesema Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 1985 inayolitaka Jeshi la Polisi kutomshikilia mtu kwa zaidi ya masaa 24 bila kufikishwa Mahakamani.

Vimelitaka Jeshi la Polisi kuheshimu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 15 inayotoa haki kwa kila mtu kuwa huru na kuishi kama mtu huru.

Chapisha Maoni

0 Maoni