Mstahiki Meya wa Ubungo Boniface Jacob aeleza Ubungo mpya aitakayo

Meya wa Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam, Boniface Jacob amesema kuanzia mwezi ujao wataanza  oparesheni ya kukusanya mapato yatakayokwenda kwenye miradi ya maendeleo.

Jacob alitoa kauli hiyo juzi baada ya kukakibidhi msaada wa Sikukuu ya Krismasi zenye thamani ya Sh2 milioni kwa makundi mbalimbali wakiwamo watu wasiojiweza.

Miongoni mwa zawadi hizo ni mbuzi tano, mchele kilo 200, juisi na guni la viazi.

Alisema halmashauri hiyo ni mpya na bado hawajajua mapato yanayokusanywa kwa mwezi ingawa lengo ni kufikia Sh36 bilioni kwa mwaka.

Chapisha Maoni

0 Maoni