Mwigulu Nchemba atembelea Wasafi, aahidi kuimarisha ulinzi wa kazi za wasanii

Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba wiki hii alitembelea ofisi ya WCB iliyopo Sinza Mapambano jiji Dar es salaam na kujionea uwekezaji uliofanywa na label hiyo ambayo ipo chini ya Diamond Platnumz.

Waziri huyo kijana aliweza kuzungumza na viongozi wa label hiyo na kuangalia namna ambavyo serikali inaweza kudhibiti wizi wa kazi za wasanii.

Baada ya kumaliza mazungumza hayo, Waziri Nchemba kupitia instagram yake aliandika:

    #Wizi wa kazi za wasanii #Jeshi la polisi kuongeza nguvu

Pia alisema kuwa serikali haitasita kuwapa msaada pale watakapokwama na kuhitaji usaidizi wa serikali.

Chapisha Maoni

0 Maoni