Nay wa Mitego awashukia wanamziki wanaofanya hiphop ngumu, adai wajikusanye waje washindane naye

“Hao wanaosema mimi sio mwana hip hop nipeleke nao kwenye show moja, hao walionitoa kwenye list ya hip hop. Tena ninachokuomba waandalie show yao Leaders waweke 16, niandalie show yangu Escape 1 peke yangu. Nakuambia wakipata watu kweli hip hop yao ina nguvu. Wote unaowasikiaga waandika, wanakesha, wanatweet ‘Nay si mwanahiphop’ wajikusanye kwenye show yao moja halafu mimi nipige pale upande wa pili halafu tuone nani atapata watu,” Nay aliiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“Wewe unakesha unanitukana kwenye mtandao wakati mimi nikiamua asubuhi naenda kununua gari mpya, nikiamua naenda kununua kibanda chenu kile cha familia mimi ninakinunua halafu wewe unaenda kukaa unanitukana kwenye mitandao, siwezi kukasirika,” amesisitiza Nay wa Mitego

Chapisha Maoni

0 Maoni