Prof. Lipumba azuiliwa kwenda Pemba

Chama cha CUF mkoani Pemba kimesema Lipumba asije thubutu kufanya ziara ya kichama huko Pemba Kama tetesi zinazoelezwa ni kweli.


Uongozi huo kupitia taarifa ya habari saa mbili usiku ITV leo wamesema Lipumba anayo haki ya kwenda Pemba Kama mtanzania mwingine kufanya shughuli zake binafsi bila kuvunja sheria kwa mujibu Wa katiba lakini sio kuja kujihusisha na CUF.

Wameongeza kusema anaweza kuja Pemba na kufikia katika hoteli yeyote Kama wasaliti wengine wanavyo Fanya lakini asije tembelea matawi au ofisi za wilaya au mkoa za chama hicho.

Kwahali ilivyo sasa naona lipumba ataendelea kujifungia Buguruni tuu akilindwa na ccm maana wana CUF wamechoka usaliti.

Chapisha Maoni

0 Maoni