TFF yakanusha kupokea taarifa kutoka FIFA

Ile barua Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuwa limerudisha majibu ya rufaa ya Simba na kusema, matokeo yanaendelea kubaki kama yalivyo, imeelezwa ni famba.


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema haijapokea barua hiyo.

Msemaji wa TFF, Alfred Lucas ameiambia SALEHJEMBE kwamba hakuna barua hiyo.

“Niko nje ya ofisi, lakini nimeulizia ofisini inaonekana hakuna barua kama hiyo iliyopokelewa,” alisema.

“Sijui labda tuendelee kusubiri, kama kuna kitu nitakujulisha ila hadi sasa hakuna barua.”


Chapisha Maoni

0 Maoni