Ya Davido na Sony, sasa Ali Kiba

Label ya sony imekuwa ikilalamikiwa jinsi inavyotreat wasanii mbalimbali wanaotokea Africa, pia imekuwa ikihusishwa na uuaji wa vipaji vingi barani hapa


Baada ya mwaka jana, Msanii Davido kusoteshwa na kuzuiliwa kutoa nyimbo mpya na label yake hii ya sony baana ya kusain nao mkataba mpaka hali hii ikazua maswali na mtafaruku mkubwa juu ukimya wake wa muda mrefu isivyo kawaida, sasa hali hiyo imemkuta msanii wetu kipenzi cha watu ALIKIBA

Ni zaidi ya mwaka sasa tangu alikiba alipoachia smash hit yake iliyotamba sana "Aje"
baada ya hapo ukimya umetawala pasi na washabiki wake wasijue nini cha kufanya

inasemekana sasa Sony ndio wanamuhenyesha nguli huyu na kusubilisha kutoa ngoma mpya mpaka hapo watakapoamua!

Hili jambo litakuwa na impact mbaya kwa Kiba, hasa ukiangalia jinsi ushindani ulivyo kwa sasa katika game yetu hapa nchini na afrika kwa ujumla

Sony, tuachieni msanii wetu atupe Raha "tumechoka" sasa

Chapisha Maoni

0 Maoni