Mwandishi wetu amefika katika kijiji hicho cha Mwelezo na kukuta baadhi ya wananchi waliopata kipigo wakimlalamikia kamanda wa sungusungu wa wilaya ya Shinyanga kualika kundi la watu na kuamrisha yasomwe majina ya baadi ya watu kwa madai kuwa ni wahalifu na kuadhibiwa kwa kuchapwa viboko kosa ambalo wamedai limetokana na wao kudai kusomewa mapato na matumizi katika mikutano ya kijiji kwa muda mrefu bila mafanikio.
Akitoa kauli ya kumsimamisha kazi mwenyekiti wa kijiji cha Welezo bw.Salum Shabani mkuu wa wilaya ya Shinyanga Bi.josephine Matiro amesema amelazimika kuunda uongozi mpya wa jeshi la sungusungu pamoja na kumteua Bi.Janeth Kurubone kukaimu nafasi ya uenyekiti hali ambayo imemlazimu mwenyekiti huyo aliyesimamishwa kuondoka katika mkutano huo mara moja kwa hofu ya kupigwa na wananchi waenye hasira kali.
Kulwa Masanja ni Kamanda wa sungusungu wa wilaya ya Shinyanga anayetuhumiwa kualika kundi la sungusungu zaidi ya 800 kuwaadhibu wananchi wa kijiji hicho cha welezo amelazimika kuomba msamaha na kudai kuwa alichomekwa bila kujua huku mbunge viti maalum wilaya ya Shinyanga Mh.Aza Hilali akikiri kuwepo kwa migogoro ya muda mrefu inayosababishwa na baadhi ya viongozi wa serikali ngazi ya kata vijiji na vitongoji kutokuwa waaminifu kwa wananchi.
Chanzo: itv

0 Maoni
TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA