AJALI MBAYA YA NOAH YATOKEA HUKO TUNDE MKOANI SHINYANGA


Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba watu zaidi ya 10 wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha gari aina ya Noah iliyokuwa inatoka Nzega kuelekea Tinde na Lori aina ya Scania lililokuwa linatoka Kahama kuelekea Dar es salaam.


Ajali hiyo imetokea majira ya mbili kasorobo usiku leo Jumapili,November 06,2016 katika eneo la Nsalala kata ya Tinde mkoani Shinyanga.

"Waliopoteza maisha ni wengi sana,wapo zaidi ya 10,ajali inatisha",kimesema chanzo chetu cha habari .

Majeruhi wanakimbizwa hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Chapisha Maoni

0 Maoni