ARUSHA: Wimbi la utupaji watoto wachanga wenye umri wa siku 1-12 laongezeka

Wimbi la utupaji watoto wachanga wenye umri wa siku moja hadi kumi na mbili kwenye maeneo ya karibu na hospitali, mitaroni jalalani na kando ya vituo vya kulelea yatima limezidi kushika kasi katika mkoani wa Arusha ambapo kwa kipindi kifupi inadaiwa zaidi ya watoto themanini wameokotwa na wasamaria wema na kupelekwa kwenye vituo vya kulelea watoto .


Katika uchunguzi uliofanywa kwenye baadhi ya vituo vya kulelea watoto wenye mazingira magumu umegundua idadi hiyo ni kwa vituo viwili tu vya Samaritani na Faraja ambako wasamaria wema waliookota watoto waliwapeleka akiwemo mtoto wa siku kumi na mbili anayedaiwa kuokotwa hivi karibuni pembezoni mwa hospitali ya Seliani huko Ngaramtoni huku walezi wa vituo hivyo wakidai wamekuwa wakishirikana na jeshi la polisi pamoja na maafisa ustawi wa jamii wanapofikishiwa watoto wanaookotwa.

Wakizungumzia matukio hayo baadhi ya wasamaria wema wamesema tabia hiyo inatakiwa kukomeshwa kwani kitendo hicho kinawanyima watoto haki ya kuishi na kuwataka watanzania kuwa na tabia ya kuwasaidia watoto hao wasiyo na hatia.

Baadhi ya watoto waliyotelekezwa na kuokotwa na wasamari wema miaka ya nyuma ambao hivi sasa wamekuwa na kumaliza elimu ya msingi wameeleza kitendo hicho kinavyo waumiza na kuwataka watanzania kuwaona kwa jicho la huruma.

Chapisha Maoni

0 Maoni