Ripoti ya utafiti wa TWAWEZA yaonesha asilimia 92 ya watanzania wanataka Bunge live.

UTAFITI: Ripoti ya Taasisi ya Twaweza yaonyesha asilimia 92 ya wananchi wanapendelea vipindi vya Bunge kuonyeshwa moja kwa moja.

Pia katika utafiti huo asilimia 65 wanasema Vyombo vya Habari havijawahi au kama vimeshawahi, ni mara chache sana vimekuwa vikitumia vibaya uhuru wake kwa kutangaza vitu ambavyo si vya kweli.

Utafiti pia unaonyesha wananchi wanaunga mkono kwa kiasi kikubwa uhuru wa maoni na kupata taarifa. Karibu wananchi wote (95%) wanasema wananchi wawe huru kuikosoa serikali pale ambapo wanaona imekosea.

Chapisha Maoni

0 Maoni