Yanga hawapendi ujinga wanapoona vitu vizuri

Related image
Yanga wamekuwa hawajiulizi mara mbili waonapo kitu kizuri na wanapokihitaji huwa hawasiti kutumia pesa ili kukipata kitu kizuri.



Baada ya mchezo wa JKU kuisha kwa Yanga kufungwa 2 Kwa 0 na mchezaji Emmanuel Martin kupachika bao zote 2,Taarifa za ndani zilidai kocha Lwandamina alivutiwa na uwezo wa mchezaji huyo.

Mtembeleaji wa MAHENGA BLOG Sasa kama ulikuwa hujui baada ya mechi Yanga walijipanga kufanya mazungumzo na mchezaji huyo aliyekuwa na mkataba na JKU na mambo yalimalizika kiwepesi sana.

Lakini kulingana na katibu mkuu wa JKU alisema wazi kuwa Yanga wametoa pesa ya kutosha na wamemalizana kabisa na Yanga, huku akisema mambo ya mchezaji huyo yanaenda kuwa mazuri 

Kwani Mshahara anaoenda kuupata Yanga aliweka wazi kuwa siyo mara 2 ya mshahara wa JKU Bali ni mara 10 ya mshahara aliokuwa analipwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni