Simba Watoka Matopeni...Warejea Rasmi Kimataifa

Klabu ya soka ya wekundu wa msimbazi ya simba imetwaa ubingwa wa kombe la shirikisho la TFF baada ya jioni ya leo kuinyuka Mbao FC bao 2-1 kwenye mechi ya fainali iliyopigwa kunako dimba la Jamhuri mkoani Dodoma.

Kwa ushindi huo Simba imejinyakulia milioni 50 na kujikatia tiketi ya kucheza kunako michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika kwa mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 2012/13, huku mshindi wa pili akiambulia patupu zaidi ya medali kwa kuwa hakuna zawadi ya fedha kwa mshindi wa pili wa michuano hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni