Aliyewakatakata Watalii Mapanga Zanzibar Akamatawa na Polisi


Polisi imemkamata mtuhumiwa anayedaiwa kuwajeruhi watu sita kwa kisu mjini Zanzibar Mei 29.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa jana saa 8:30 mchana akituhumiwa kuwajeruhi watu hao katika mgahawa wa Lukmaan uliopo Mkunazini mjini Zanzibar.

Katika tukio hilo, raia wa kigeni wanne na Watanzania wawili walijeruhiwa maeneo mbalimbali ya miili yao kwa kuchomwa kwa kisu.

Mtuhumiwa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Madema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali amethibitisha kushikiliwa kwa mtuhumiwa huyo.

Amesema wanaendelea kumhoji ikiwa ni hatua za awali za upelelezi.

Chapisha Maoni

0 Maoni