Amezitaka taasisi za Kiislamu nchini kukataa maagizo kutoka TRA.
Pia ameishtumu Serikali ya awamu ya 5 kuwa inawanyima waumini wa dini ya kiislamu nyadhifa katika teuzi mbalimbali na amesema kuwa baadhi ya Waislamu wamekuwa wakiondolewa nafasi zao serikalini sababu ya dini yao.
Ameongeza kwa kuitaka Serikali ibadilishe sheria ya ugaidi nchini kwa sababu ni kandamizi na Waislamu wengi wamekuwa wakikamatwa kwa kisingizio cha kuwa magaidi na hawapelekwi mahakamani na mpaka sasa kuna baadhi wako jela bila kufikishwa mahakamani, ametoa mfano wa masheikh wa Zanzibar wanaoshikiliwa kwa muda mrefu bila kufikishwa mahakamani.
0 Maoni
TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA