CHAMA cha Demokrasia na maendeleo (Chadema), kipo katika mkakati mzito
wa kuhakikisha Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi(CCM),inayoanza kikao
chake leo jijini Dar esSalaam, kinampitisha Dotto Msawa,ambaye ni diwani
wa Kigamboni CCM,kuwa mgombea wa nafasi ya Umeya wa Manispaa mpya ya
Kigamboni kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya kuwa na turufu katika
maamuzi mbali mbali ya jiji la Dar sSalaam kwa mambo yatakayohitaji
uamuzi wa kupiga kura
Taaria za uhakika toka ndani ya Chama hicho zinadokeza kuwa,tayari
mkakati huo unasimamiwa na watu wa Karibu wa waziri mkuu aliyejiuzulu
Edward Lowasa kwa kuzingatia ukaribu wao wakati Lowasa alipokuwa CCM
Inaelezwa kuwa moja ya mikakati ya kuhakikisha kamati kuu inampitisha
Msawa, ni pamoja na diwani huyo kushambuliwa kwa maneno na kuibuliwa kwa
kashfa zake mbali mbali kupitia gazeti la Tanzania Daima linalomilikiwa
na mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe.
“Chadema kwa Manispaa ya Kigamboni haina chake kwani madiwani wa Ukawa
ni wachache hivyo mkakati wao umelenga katika dhana nzima ya Rais
Magufuli kuwapitishia mtu wao kupitia kauli yake kuwa ukiona wapinzani
wako wanamshambulia sana mtu wako basi huyo ndiyo umpe nafasi na sasa
hivi kama unafuatilia utajua namna mkakakti huo ulivyofanikishwa kwa
kina na gazeti la Tanzania Daima”kilidokeza chanzo cha habari hizi .
Msawa anayetajwa kuwa swahiba wa Karibu wa Edward Lowasa, katika mkakati
huo anatajwa kuwatishia gazeti la Tanzania Daima kuwa atawapeleka
mahakamani kwa kumchafua lengo lilikwa ni kukuza mjadala wa jina lake
kabla ya kamati kuu ya CCM haijafanya uteuzi wa jina la mgombea umeya wa
Kigamboni
Kwa zaidi ya wiki tatu sasa gazeti la Tanzania Daima limekuwa
likiaandika taarifa zinazomhusu Dotto Msawa ikiwa ni pamoja na kuweka
vielelezo vya namna alivyofikishwa mahakamani mkoani Morogoro Mwaka 2011
akihusishwa katika wizi wa gari


0 Maoni
TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA