DC Gambo kukabidhi pikipiki 200 zisizokuwa na riba kwa bodaboda kesho.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo mapema leo amekutana wa waendesha boda boda 200 watakaonufaika na mradi wa kuwainua vijana kiuchumi katika Jiji la Arusha kwa kupatiwa Pikipiki zisizokuwa na riba.


Mhe. Gambo amekutana na vijana hao ili kukamilisha taratibu za mwisho na kuangalia masuala ya usalama kabla hawajakabidhiwa Pikipiki hizo.
Katika Kikao hicho vijana hao wamekubalina kwa Pamoja kwamba watarejesha Tsh 7,000 kwa siku na pia na kwa atakayeweza kwa wiki Tsh 49,000 ama kwa Mwezi itakua Tsh210,000.


Pia walikubaliana kwamba ni ruksa kwa yeyote atakayeweza kulipia zaidi ya kiasi icho ili aweze kumaliza mkopo wa Pikipiki yake na aweze kumilikshwa Pikipiki hiyo.
Haikatazwi kwa mtu yeyote kuleta zaidi ya Tsh 7,000 kwa siku ili uweze kumalizia mkopo wako mapema na ikitokea umekamilisha mkopo huo hata kwa miezi miwili unamilikishwa Pikipiki alisema Mhe. Gambo.


Vijana hao pia walihoji kuhusu service ya Pikipiki hizo na Mwakilishi wa Kishen Enterprises Ltd ambao pia ni mawakala wa Pikipiki aina ya Toyo Mkoani hapa alisema Pikipiki hizo zina warrant wa meizi sita na endapo zitapata hitilafu kwenye Engine katika kipindi hicho wataweza kuifanyia matengenezo bila gharama yeyote au kubadilishiwa Pikipiki nyingine.
Kwa hesabu za kawaida vijana hawa watarejesha Tsh 2,135,000 kwa mchanganuo ufuatao:
Tsh 2,000,000 ni Bei ya Pikipiki


Tsh 135,700 ni gharama ya Bima Kubwa hivyo
Vijana hao watarejesha Tsh 7,000 X siku 305 = 2,135,000.
Tunaposema watalipia kwa kipindi cha mwaka mzima tunaamisha siku 60 zitakua kwa ajili ya service na dharura nyingine na siku 305 ndio watakazoleta marejesho Alimalizia Mkuu wa Mkoa.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema Pikipiki hizo zitakabidhiwa siku ya Jumamosi tarehe 10/12/2016 saa nne Asubuhi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Wote Mnakaribishwa kushuhudia Tukio hili la Kihistoria

Chapisha Maoni

0 Maoni