Goli la Mane laibeba Liverpool

Wachezaji wa Liverpool wakishangilia ushindi


Majogoo wa Anfield Liverpool wameendelea kuwa na msimu mzuri katika ligi kuu ya England baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa dabi dhidi ya Everton.

Mshambuliaji nyota wa Majogoo hao Sadio Mane ndie aliyeipatia timu yake alama tatu muhimu baada ya kufunga bao pekee la ushindi, katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Goodson Park.

Kwa ushindi huo Liverpool, wanapanda mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi wakiwa na alama 37 huku wakiwa wamecheza michezo 17 ya ligi.

Chelsea wanasalia katika nafasi ya kwanza wakiwa na alama 43.

Chapisha Maoni

0 Maoni