Maxence Melo: Mtandao wa jamiiforums haujatetereka, bado upo ngangari


Baada ya kuchiwa leo kwa dhamana Mwanzilishi mwenza wa JamiiForums, Maxence Melo amesema mtandao wa JamiiForums haujatetereka na bado uko ngangari na amewataka watumiaji wote wa mtandao huo waondoe hofu kwa kuwa taarifa zao za siri ziko salama.



Pia amesema hana ugomvi wowote na vyombo vya dola na ana imani na mahakama za hapa nchini kuwa zitamtendea haki katika kesi yake.

Amewataka wananchi wote bila kujali itikadi zao kuendelea kupigania uhuru wa kusema na kutoa maoni, pia amevishukuru vyombo vyote vya habari na wanahabari kwa kumuunga mkono kipindi chote alipokuwa mahabusu.

Chapisha Maoni

0 Maoni