Serikali yawakana waajiriwa wapya 3,000 wa mwezi June 2016. Yachukua maamuzi ya kuwafuta kazi

Serikali imesema haitambui mkataba wowote wa ajira uliotolewa baada ya Mei Mosi, kwa kuwa suala hilo lilizuiwa kuanzia siku hiyo ili kupisha uhakiki wa watumishi hewa.


Msimamo huo ulitolewa jana na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro alipotoa ufafanuzi kuhusu wataalamu wa mifugo walioajiriwa Mei 2, na taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba amefuta ajira za walioajiriwa Juni.

“Ajira zote zilisitishwa Mei Mosi kupisha msako wa watumishi hewa. Yeyote aliyepewa barua ya ajira baada ya hapo ni kama hakupewa kitu,” alisema Dk Ndumbaro.

CHANZO: Mwananchi


Chapisha Maoni

0 Maoni