Tupunguze "kuisimanga" ATCL, haijengi zaidi ya kukatisha tamaa

Hizi ndege hata marubani wanaziogopa!!!Maana zipo "kisiasa" sana.Kila mtu anatafuta pa kupatia "kick" linapokuja suala la ATCL.Kilichotokea Kisongo ni jambo la kawaida sana ktk usafiri wa anga.


Hapo ni suala la kawaida sana,wakati wa kutua rubani alikuwa anataka kupiga turning ili aingie Apron(sehemu ya maegesho ya ndege)kwa ajili ya kushusha abiria,lkn bahati mbaya tairi moja la nyuma likatoka nje ya runway.

Sasa kwa sbb hizi ni ndege mpya;jamaa akaona isiwe tabu,ni bora asubiri "Towing Car" ili aweze kuitoa.Angeweza kuitoa hata kwa ku-tax,lkn amechukua tahadhari ili kuepuka lawama.

Na kwa sbb uwanja wa Kisongo ni 12hrs,hufunguliwa na kufungwa wakati wa mawio(sunrise) na wakati wa machweo(sunset),kwa muda iliofika Kisongo na kutaka kuondoka ndege isingeweza sbb muda wa kufungwa uwanja ulishafika,na Kisonge haina taa za sehemu ya kutua na kurukia,kama ingalikuwapo "dear bombadia" ingerudi Dsm usiku kwa usiku.

Hali hii ipo Mtwara,Kigoma,Tabora na hata Mbeya.Ndio maana kuna safari ikitokea itilafu kidogo tu na ikafika saa kumi jioni Fastjet bado ipo Dsm haiwezi kwenda tena Mbeya.

Safety First,hiki ndicho rubani kazingatia,angeweza kulazimisha kukata kona na kuitoa,lkn alitaka kuhakikisha kuwa abiria wote wanashuka kwanza ili kupunguza uzito.Yangetokea mengine ndio watu wangelaumu sana.

Incidence za kubasti tairi,kuchepuka nje ya runway au taxway ni za kawaida sana,ni kwa sbb huwa haziripotiwi au ni kwa vile zimetokea kwa ATCL ndio maana zinashika kasi na heading mitandaoni.
Rubani kafanya maamuzi sahihi...

Na hii ni incidence ya kawaida sana ktk usafiri wa anga.Hapa juzi kati huko Nairobi ndege ilipata tatizo kwenye Runway na uwanja ukafungwa zaidi ya masaa 6,ndege zote za Jomo Kenyata zikawa diverted KIA na Dsm hadi uwanja ulipofunguliwa.

Siku kadhaa zilizopita zililetwa habari za Oman Air kupata mpasuko wa tairi huko Dsm.Waarabu wa Oman walikaa kimya huku wakiendelea na uchunguzi,hawakupiga mayowe ili wasipoteze abiria wa ndege zao ambao wamekuwa wakizitumia kufika Asia na mashariki ya mbali.Kusafrisha mahujaji nk.Walikaa kimya sbb,basti ni kitu ya kawaida,na kwao ndege ni sehemu ya utalii na kipato cha nchi.Sasa sisi kuchepuka tu kwenye taxway/runway ni maneno ya kejeli tupu.

Masaa sita ni mengi;kwanza yanaonyesha pengine nchi husika haijajiandaa kukabiliana na dharula,majanga ya moto na ajali.Lakini vyombo vya Kenya wala havikushobokea habari hii,ilipita kimyakimya sbb wanajua madhara yake.Hii si "habari" kwa maana ya ndani ya Taifa la kwao.Linawashushia heshima ya utayari ktk majanga na uokozi.Wakaipiga "pini" na kujadili mambo mengine.

Sisi Bombadia rubani kafanya tahadhari ya kuepusha majanga kwenye "landing gears" basi kila mahali usiku huu n maneno na "kuiponda" ATCL!!Ebooooo!!Tabia gani hii ya kutokilinda vya kwenu?Ndege haina "side mirror",ilimpasa kujiridhisha ili kuiweka ndege ktk sehemu salama.Lakini watu wameanza kusema na mengine ambayo hata hayapo.

Hii ni kitu ya kawaida,ndio maana kuna incidence na accident!!Ila kwa sbb ni ATCL,watu wataongea sana saanaaa.Lkn hao hao wapiga kelele ndio wa kwanza kukuomba uwafanyie booking ya ATCL.Loooh!!Pole sana ATCL...Unaonekana "yatima" hata ktk ardhi ya mama yako Tanzania.Huu sasa sio ukosoaji,ni MASIMANGO!!Kutwa kucha kuisimanga ATCL...Duuuh!!

Chapisha Maoni

0 Maoni