AZIMIO LA DODOMA, BAVICHA NA CHASO WAJA NA MAPENDEKEZO MATANO KWA VIJANA NA SERIKALI

Akitangaza maadhimio hayo katika kongamano lililofanyika katika ukumbi wa African Dream ulioko mjini Dodoma leo tarehe 23 akiahirisha kongamano hilo, Katibu Mkuu wa vijana na katibu Mwenezi Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Edward Julius ameyatoa mapendekezo hayo na kutoa rai kwa vijana kutonunulika kwa urahisi na chama tawala. Mapendekezo hayo pia yameungwa mkono na Umoja wa Wanafunzi Chadema (CHASO) kama maridhiriano ya
nini kifanyike. Makubaliano hayo matano ni kama ifuatavyo;

1.      1. Serikali isiingilie mihimili mingine ikiwa ni pamoja na Bunge na hivyo vikao vya Bunge vioneshwe moja kwa moja na Shirika la utangazaji la taifa (TBC).
2.   2   Kueneza chachu hii nchi nzima kwa kujitolea na hivyo kutoa rai kwa vyombo vya ulinzi na usalama kutowanyima haki yao ya msingi ya makusanyiko ya hadhaara,
3.      3 Serikali iongoze kwa kufuata sharia na kanuni za nchi zilizoainishwa kwenye katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kutaka katiba mpya itolewe.
4.     4 Kuendesha harakati za kudai mabadiliko kwa kujitolea.
5.      5 Serikali isipotenda haki, basi haki itapatikana barabarani-maandamano.

Pamoja na mapendekezo hayo, Mh. Julius ametoa pia wito kwa vijana kufanya kazi kwa kujitolea na bila uoga wa aina yoyote.

Chapisha Maoni

0 Maoni